Madaktari Bingwa wa Mifugo kisiwani Pemba wamefanikiwa kumfanyia upasuaji Ngombe alie kwama mtoto wakati wa kujifungua kwa kumzalisha kupitia ubavuni .
akizungumza na Pemba upembani Mkuu wa mradi wa kuwahudumia wakulima na wafugaji kisiwani Pemba Asha Omar Fakih amesema upasuaji huo umefanyika kwa mafaniko makubwa kwa kumzalisha ndama huyo akiwa mzima na badae wakamshona ngombe huyo
alisema cha faraja zaidi nikuwa tukio hilo liliwakutanisha wahudumau wa mifugo ambao wanapewa mafunzo ya kuzalisha ilinao baadae waweze kufanya upasuaji pindi kesi yaonahio ikitokea.

No comments:
Post a Comment